Posts

Showing posts from May, 2020

MSAMAHA WA KWELI?

JINA LA HADITHI FUPI: MSAMAHA WA KWELI ? MWANDISHI: SAID KAITA FACEBOOK PAGE: Saidikaitastories.com BLOG: Saidikaitastories MAWASILIANO: 0783372139 E-MAIL: Saidikaita7@gmail.com        Usilolijua ni sawa na usiku wa giza nene. Ni msemo ambao mara chache hutumika katika ndimi za watu ila huwatokea tu muda ambao jambo husika limeshatendeka pia kuwa na uhakika nalo.        Usiku ulioambatana na sauti za mbu zililizunguka eneo alilokuwa amelala Ahata. Sauti zilizojawa hasira kila mmoja wao akiwa anatafuta kitoweo. Kwa ukali wa sauti zile ulisikika kama mtu akiwa anapiga kinanda kwa utaalamu na hakuna ambaye angeweza kulala kwa sauti zile. Sauti ya makofi ilikuwa ikisikika kila mahali “Paaa... Paaa” kila mtu alikuwa akijihami asing'atwe. Ahata alikuwa amelala chini ya kalavati akiwa amejifunika na mfuko wa kubebea uchafu. Mbalamwezi iliyokuwa iking'aa angani kwa namna yake iliweza kutoa nuru na kufanya watu wengi waliokuwa wamelala pale ku...

SIRI

HADITHI FUPI JINA LA HADITHI: SIRI MWANDISHI: SAID KAITA MAWASILIANO: 0783372139 E-mail: Saidikaita7@gmail.com FACEBOOK PAGE: Saidikaitastories.com Nyota njema huonekana alfajiri. Ni fikra ilojaa kwa kila mwanadamu aliyepevuka akili. Lakini Jose kwake sidhani kama atakuwa ameiona hiyo nyota njema. Jose akiwa amesimama huku anasikiliza usia kutoka kwa baba yake anayeonekana yuko kitandani akiwa amelala na afya yake ikiwa imedhoofika sana. “Jose… mwanangu… ni muda mrefu nikiwa nai… angalia …. dunia kwa ma…ma… chungu kwa ugonjwa niliokuwa nikisu… sumbuliwa. Mmejaribu kunitibu kwa njia yoyote ile lakini juhudi zenu zote naona kama zinaenda kugonga ukuta”. Jose akawa ameshtuka na kumuuliza baba yake. “Baba mbona kama unanitisha? …”. Ilikuwa ni vigumu sana kwa Jose kuweza kuelewa nini hasa kilichokuwa kikiendelea kwa baba yake ambaye kwa hali halisi ni kwamba alikuwa akienda kuaga maisha yake ya dunia ya tatu ili kwenda kuonana na maisha ya dunia   nyingine. Baba Jose alizungumza...